Saturday, February 28, 2015

UEFA YAILIMA FAINI HULL KWA KUKIUKA SHERIA YA MATUMIZI YA FEDHA, LIVERPOOL YASEVU.

KLABU ya Hull City imetozwa faini ya paundi 145,000 na Shirikisho la Soka La Ulaya-UEFA kwa kukiuka masharti ya matumizi ya fedha huku Liverpool wao wakitoka safi baada ya ukaguzi. Meneja wa Hull Steve Bruce anadhani kuwa adhabu hiyo wamepata kutokana na gharama walizotumia wakati wakijaribu kupatanda daraja msimu uliopita. Hull watalazimika kulipa faini nyingine ya paundi 290,000 kama wakikiuka masharti hayo msimu ujao. Bruce amesema taarifa hizo ni mbaya kwao kwani sababu kubwa ya wao kuingia katika uchunguzi huo ni kwasababu ya mikakati yao ya kupanda Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment