Saturday, February 28, 2015

ANCELOTTI AWAPUUZA BARCELONA NA KUDAI KILA MECHI NI MUHIMU KWAKE.

MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti amesema mechi tatu za La Liga zinazowakabili ni muhimu kama ulivyo mchezo dhidi ya Barcelona maarufu kama Clasico utakaochezwa Machi 22 mwaka huu. Kwasasa Madrid ndio wanaongoza msimamo wa La Liga wakitofautiana na Barcelona walioko nafasi ya pili kwa alama nne ambao watachuana nao katika Uwanja wa Camp Nou katika mchezo utakaotoa muelekeo wa bingwa wa msimu huu. Hata hivyo kabla ya mchezo huo, Ancelotti amesema wana michezo mingine mitatu dhidi ya Villarreal, Athletic Bilbao ba Levante ambayo inabidi waizingatie kabla ya kuanza kuwafikiria Barcelona. Ancelotti amesema michezo hiyo ni muhimu kwani kama wakipoteza alama wanaweza kuhatarisha matumaini yao ya kunyakuwa taji msimu huu.

No comments:

Post a Comment