Saturday, February 28, 2015

HERRERA ATAMBA KUJA KUWA MCHEZAJI MUHIMU WA UNITED SIKU ZA USONI.

KIUNGO wa klabu ya Manchester United, Ander Herrera amekataa kulazimisha kupewa nafasi katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo chini ya meneja Louis van Gaal. Baada ya kununuliwa kwa fedha nyingi kutoka Athletic Bilbao katika kipindi cha majira ya kiangazi msimu uliopita, nyota huyo wa kimataifa wa Hispania amekuwa akianza kama mchezaji wa akiba mara nyingi zaidi kuliko katika kikosi cha kwanza. Pamoja na hayo Herrera amekubaliana hali hiyo kwani anajua itachukua muda mpaka aweze kushawishi na kupata nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza mara kwa mara. Akihojiwa Herrera amesema anapenda kucheza mara nyingi kadri iwezekanavyo akiwa United lakini hawezi kulazimisha kwakuwa anajua itachukua muda kumshawishi kocha. Herrera amesema anataka kushinda mataji na United na pia anataka kuwa mchezaji muhimu wa timu hiyo hivyo anadhani katika kipindi sio kirefu anaweza kufikia malengo hayo.

No comments:

Post a Comment