Thursday, February 26, 2015

STERLING KARIBUNI KUSAINI MKATABA MPYA LIVERPOOL.

MSHAMBULIAJI mahiri wa Liverpool, Raheem Sterling ana matumaini ya kusaini mkataba mpya na timu hiyo hivi karibuni na kudai kuwa Anfield ni mahali pazuri kwa wachezaji chipukizi ili waweze kukua katika Ligi Kuu. Mkataba wa sasa wa Sterling unamalizika mwaka 2017 na mazungumzo na mkataba mpya bado hayajafikia muafaka. Hivi karibuni meneja wa Liverpool, Brendan Rogders alidai kuwa klabu hiyo imepanga kumpa Sterling mwenye umri wa miaka dili nono. Sterling amesema anazungumza na wawakilishi wake kila siku na wamemuhakikishia kuwa yeye atilie mkazo soka na kuwaachia wao mambo mengine kwani watayamaliza hivi karibuni. Nyota huyo amesema kwasasa anatilia mkazo kuisaidia Liverpool kushinda mechi zake na ni matumaini yake mazungumzo ya mkataba wake mpya yatamalizika haraka.

No comments:

Post a Comment