Thursday, February 26, 2015

LIPPI AACHANA NA GUANGZHOU EVERGRANDE.

KLABU ya Guangzhou Evergrande ya China imethibitisha kuwa kocha mkongwe Marcello Lippi ameachana na klabu hiyo. Kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Italia na klabu ya Juventus alichukua mikoba ya kuinoa timu hiyo inayoshirikis Ligi Kuu ya China Mei mwaka 2012 kwa mkataba wa miaka miwili na nusu wenye thamani ya euro milioni 30. Lippi ameingoza klabu hiyo kushinda mataji manne ya ligi na taji moja la Kombe la FA la nchi hiyo lakini mafanikio yake makubwa yalikuja wakati alipoiwezesha timu hiyo kushinda taji la Ligi ya Mabingwa barani Asia maka jana. Kocha huyo sasa ndiye pekee aliyewahi kunyakuwa mataji ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Asia. Lippi raia wa Italia alikuwa amesaini mkataba ambao ungemalizika mwaka 2017 Februari mwaka jana lakini alitangaza kustaafu ukocha Novemba na kupewa nafasi kama mkurugenzi wa michezo wa timu hiyo.


No comments:

Post a Comment