Thursday, February 26, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: MAN UNITED YATENGA PAUNDI MILIONI 30 KWA AJILI YA WINGA WA WOLFSBURG, LIVERPOOL, UNITED WAKABANA KOO KWA DANILO.

KATIKA habari za tetesi za usajili ambazo zimepamba vichwa vya habari vya magazeti na mitandao mbalimbali Ulaya ni pamoja na winga wa klabu ya Wolfsburg Kevin De Bruyne mwenye umri wa miaka 23 kukubali kurejea katika Ligi Kuu nchini Uingereza. Taarifa hizo zinaweza kuwa njema kwa manchester United ambao wako tayari kutoa kitita cha paundi milioni 30 kwa ajili ya kumsajili nyota huyo wa zamani wa Chelsea. Klabu za Liverpool na Manchester United zimeonyesha nia baada ya kugundua kuwa beki Danilo mwenye umri wa miaka 23 amekataa kusaini mkataba mpya na FC Porto. Klabu ya Tottenham Hotspurs inataka kumsajili beki wa Monaco Aymen Abdennour mwenye umri wa miaka 25 huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Tunisia alionyesha nia ya kukubali uhamisho huo. Kiungo wa Manchester United Andreas Pereira mwenye umri wa miaka 19, anaweza kuhamia Juventus baada ya nyota huyo wa kimataifa wa Brazil kukataa kusaini mkataba mpya. Winga wa klabu ya Tottenham hotspurs Aaron Lennon mwenye umri wa miaka 27 amepania kusaini mkataba wao wa kudumu na Everton anapochezea kwa mkopo huku klabu hiyo ikiwa tayari kutoa kitita cha paundi milioni saba.

No comments:

Post a Comment