Thursday, February 26, 2015

SIMEONE ATAMBA KUWA ATLETICO INAWEZA KUBADILI MATOKEO NA KUSONGA MBELE.

MENEJA wa klabu ya Atletico Madrid, Diego Simeone amesisitiza kikosi chake kinaweza kubadili matokeo katika mchezo wao wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuchapwa bao 1-0 jana na Bayer Leverkusen. Leverkusen wamepiga hatua moja kutinga katika hatua ya robo fainali kwa mara ya kwanza toka walipofika fainali ya michuano hiyo mwaka 2002. Akihojiwa Simeone amesema Leverkusen wangekuwa wajiweka vizuri zaidi kama wangewafunga bao zaidi ya moja lakini kutokana na mchezo ulivyokuwa jana ana uhakika wanaweza kubadili matokeo hayo na kusonga mbele. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kikosi chake hakikuwa kikicheza kwa uelewano wa kutosha jambo ambalo ana uhakika litakuwa limejirekebisha mpaka utakapofikia mchezo wao marudiano nchini Hispania wiki mbili zijazo.

No comments:

Post a Comment