Thursday, February 26, 2015

KOCHA WA COLOGNE AKIRI ITAKUWA MIUJIZA KUIFUNGA BAYERN.

MENEJA wa klabu ya Cologne, Peter Stoeger amekiri kuwa watahitaji miujiza watakapocheza na mabingwa wa Bundesliga Bayern Munich kesho kutokana na ubora waliokuwa nao hivi sasa. Bayern hawajafungwa bao lolote katika michezo yao mitatu iliyopita ambapo waliigaragaza Hamburg kwa mabao 8-0 huku Jumamosi iliyopita Paderborn nao wakichabangwa mabao 6-0 na kuifanya timu hiyo kukaa klileleni kwa tofautia ya alama sita. Wakati Wolfsburg wanashika nafasi ya pili wao wakicheza na Werder Bremen Jumapili hii, timu zote hizo zimecheza hazijafungwa katika mechi zao tano za mwanzo kwa mwaka huu. Bayern atakuwa na nafasi ya kutanua pengo la alama, labda Cologne wafanye miujiza ya kuisimamisha timu hiyo. Kocha huyo amesema Bayern wao hutumia kila nafasi wanayopata na kama wakifanikiwa kufanya hivyo katika mchezo wao anadhani itakuwa ngumu kusalimika.

No comments:

Post a Comment