Thursday, February 26, 2015

NOBLE APEWA MKATABA MPYA WEST HAM.

KIUNGO wa klabu ya West Ham United, Mark Noble amesaini mkataba mpya utakaomuweka katika timu hiyo mpaka mwaka 2020 huku kukiwa na uwezekano wa kuongezwa mwaka mmoja zaidi. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27, ameshawahi kushinda tuzo ya mchezo bora wa mwaka wa timu hiyo mara mbili. Noble alijiunga na West Ham akiwa na umri wa miaka 13 mwaka 2000 na aliibuka katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo mwaka mmoja baadae. Toka wakati huo ameshacheza mecho zaidi ya 300 mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment