NAHODHA wa Chelsea, John Terry amesisitiza amebakisha miaka michache katika timu hiyo huku akidai hana mpango wa kucheza popote baada ya hapo. Terry ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu, alifunga bao la kwanza katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata katika mchezo wa fainali ya Kombe la Ligi dhidi ya Tottenham Hotspurs Jumapili iliyopita. Terry amesema kama huu ndio utakuwa mwaka wake wa mwisho katika soka anataka kuumaliza kwa mafanikio. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa klabu ndio itakayoamua juu ya mustakabali wake kama aendelee au la, lakini hana mpango wa kwenda popote kwingine. Chelsea ambao wanaongoza Ligi Kuu kwa tofauti ya alama tano wanasafiri kuifuata West Ham United kesho.

No comments:
Post a Comment