Friday, May 22, 2015

ANCELOTTI ABADO ATAKA KUENDELEA KUBAKIA MADRID.

MENEJA wa Real Madrid, Carlo Ancelotti bado anataka kuendelea kuinoa timu hiyo lakini amesema mustakabali wake utaamuliwa katika mchezo wa mwisho dhidi ya Getafe Jumamosi hii. Ancelotti aliingoza Madrid kunyakuwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita, lakini kufuatia kushindwa kunyakuwa taji la La Liga na kuondolewa katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo ya Ulaya wiki iliyopita, klabu inafikiria kumtimua na nafasi yake kuchukuliwa Rafa Benitez. Pamoja na tetesi hizo za kutimuliwa, Ancelotti ameonyesha utulivu huku akidai kuwa mustakabali wake ataujua baada ya mchezo mwisho, ingawa mwenyewe angependa kubakia. Kocha huyo amesema bado hajazungumza na klabu kuhusu mustakabali wake hivyo ataenndelea kuwa kocha mpaka itakapoamuliwa vinginevyo. Ancelotti aliendelea kudai kuwa baada ya mchezo wa Jumapili hii au Jumatatu ndio atakaa na kuzungumzia mustakabali wake na klabu na baadae ndio uamuzi utatoka kama aondoke au abakie.

No comments:

Post a Comment