Friday, May 22, 2015

NINA NDOTO ZA KUITUMIKIA BARCELONA - FEKIR.

KIUNGO wa klabu ya Lyon ya Ufaransa, Nabil Fekir amebainisha ana ndoto za kuichezea Barcelona katika siku zijazo. Fekir mwenye umri wa miaka 21 amekuwa katika kiwango bora msimu huu, akiifungia Lyon mabao 13 wakati wakipambana kugombea taji la Ligue 1 mpaka katika mwezi wa mwisho wa msimu na Paris Saint-Germain. Kiwango chake hicho kinamfanya kuhusishwa na tetesi za kutimikia Inter Milan katika majira ya kiangazi lakini mwenyewe amekiri uhamisho wa kwenda Barcelona ndio chaguo analohitaji. Akihojiwa Fekir amesema toka akiwa mdogo amekuwa na ndoto za kuichezea Barcelona na kama akipata bahati ya kucheza huko siku moja itakuwa in mafanikio makubwa kwake.

No comments:

Post a Comment