Friday, May 22, 2015

VAN GAAL SASA AMUWINDA SCHEINSTEIGER.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal yuko tayari kutumia mwanya wa Bastian Schweinsteiger kusimamisha mazungumzo ya mkataba mpya na Bayern Munich kwa kumpa ofa ya kuhamia Old Trafford. Van Gaal ambaye bado anamuwania beki wa Borussia Dortmund Mats Hummels, pamoja na madai ya klabu hiyo kuwa atabakia Signal Iduna Park, anataka kuongeza kingo mmoja mzoefu katika kikosi chake msimu ujao kutokana na Michael Carrick kusumbuliwa na majeruhi ya mara kea mara. Mazungumzo tayari yameashaanza kati ya pande hizo mbili na Van Gaal anaamini anaweza kumshawishi Schweinsteiger kujiunga nao baada ya kukataa kusaini mkataba mpya na Bayern. Akihojiwa kuhusu mustakabali wake Schweinsteiger amesema hana haraka ya kusaini mkataba mpya kwani amebakisha mwaka mmoja zaidi kabla ya huu wa sasa haujaisha. Kiungo huyo aliendelea kudai kuwa jambo la msingi kwake hivi sasa ni kuhakikisha anapona majeruhi yake ambayo yamekuwa yakimsumbua kea kipindi kirefu.

No comments:

Post a Comment