Monday, May 25, 2015

ANCELOTTI KUFANYIWA UPASUAJI WA SHINGO.

MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti anatarajiwa kusafiri kwenda Vancouver, Canada kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa shingo. Ancelotti anasubiria mustakabali wake kama atatimuliwa Madrid baada ya kumaliza msimu bila kushinda taji lolote, huku tamko rasmi la klabu likitarajiwa wakati wowote. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 55 ana mkataba ambao unamalizika baada ya msimu ujao lakini rais wa Madrid Florentino Perez anategemewa kumtimua kutokana na kushindwa kufanya vyema. Akihojiiwa Ancelotti amesema kama akiendelea kupoteza muda na kutolitibu tatizo hilo ameambiwa kuwa lineweza kukua na kumletea madhara zaidi huko mbele ndio maana ameamua kufanya upasuaji.

No comments:

Post a Comment