Thursday, May 28, 2015

AYEW KUTIMKIA ROMA.

KIUNGO wa kimataifa wa Ghana, Andre Ayew anatarajiwa kukamilisha mkataba wa miaka minne na klabu ya AS Roma akiwa kama mchezaji huru. Ayew alimaliza mkataba wake na klabu ya Olympique Marseille msimu huu, na ameamua kuchagua kwenda kwa wakongwe hao wa Italia badala ya Ligi Kuu na Bundesliga. Inaaminika kuwa Ayew aliwapa masharti Roma kuwa aataka kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya sharti ambalo limefanikishwa. Taarifa zinadai kuwa Ayew atakuwa akikunja kitita cha euro milioni tatu kila mwaka katika mkataba huo wa miaka minne atakaosaini. Ayew ameichezea Marseille kwa zaidi ya 10, klabu ambayo ndio imemkuza toka akiwa mdogo.

No comments:

Post a Comment