Thursday, May 28, 2015

MICHUANO YA AFRIKA YA U-23 KUANZA KUTIMUA VUMBI NOVEMBA 28.

SHIRIKISHO la Soka la Afrika-CAF, limethibitisha kuwa Novemba 28 mwaka huu kuwa tarehe rasmi ya michuano ya Ubingwa wa Afrika kwa vijana chini ya miaka 23, itakayofanyika huko Senegal. Michuano hiyo ya pili ya vijana mara ya kwanza ilikuwa imepangwa kufanyika huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo lakini ilibadilishwa baada ya wenyeji hao kujitoa kutokana na kukabiliwa na uchaguzi mkuu kipindi hicho. Senegal ambao hivi karibuni waliandaa michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 20, ndio wamepewa uenyeji wa kuandaa michuano hiyo ambayo wachezaji wake watakuwa wale waliozaliwa baada ya Januari mosi mwaka 1993. Kamati ya utendaji ya CAF ambayo iko jijini Zurich kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA ilkutana juzi kupitisha tarehe hiyo. Michuano hiyo sasa inatarajiwa kufanyika katika miji miwili ya Dakar na M’bour kuanzia Novemba 28 mpaka Desemba 12.

No comments:

Post a Comment