Thursday, May 28, 2015

MARSEILLE YAITAKA CLUB AFRICAIN KUTOA EURO MILIONI MOJA.

KLABU ya Olympique Marseille ya Ufaransa, imeitaka Club Africain kulipa kitita cha euro milioni moja kama wanataka kumnunua Saber Khalifa kwa mkataba wa moja kwa moja. Khalifa alijiunga na Club Africain kwa mkopo akitokea Marseille na kuwa mmoja kati ya wachezaji muhimu wa timu hiyo. Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Tunisia, Africain ilituma ombi lake Marseille kutaka kumnunua Khalifa moja kwa moja hatua ambao wamejibiwa kwa kutakiwa kutoa euro milioni moja. Mkopo wa Khalifa na Club Africain unatarajiwa kumalizika mwishoni msimu huu, huku yeye mwenyewe akidai hajui hatma yake kwasasa.

No comments:

Post a Comment