Thursday, May 28, 2015

GERRARD KUCHEZA MECHI YAKE YA KWANZA GALAXY JULAI 11.

NAHODHA Liverpool anayeondoka, Steven Gerrard anatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza akiwa na klabu yake mpya ya Los Angeles Galaxy Julai 11 mwaka huu. Kiungo huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 34, anatarajia kuwepo katika mchezo wa nyumbani dhidi ya klabu ya America ya Mexico michuano ya Kombe la Kimataifa. Ofisa mkuu wa Galaxy, Bruce Arena wanategemea Gerrard kuwepo kabla ya Julai 11 kwa ajili ya kufanya mazoezi na wenzake kwa ajili ya mchezo huo. Kwasasa Gerrard yuko katika mapumziko ya msimu na wachezaji wenzake wa Liverpool, Dubai lakini anatarajiwa kuelekea nchini Marekani kuanza changamoto mpya na anatarajiwa kuwa mchezaji rasmi wa Galaxy kuanzia Julai 8 mwaka huu. Gerrard ameasaini mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo baada ya kutangaza Januari kuwa ataondoka Liverpool klabu ambayo ameitumikiakwa miaka 17.

No comments:

Post a Comment