Thursday, May 28, 2015

SEVILLA YATETEA TAJO LAO LA EUROPA LEAGUE.

KLABU ya Sevilla ya Hispania imefanikiwa kushnda taji lake la nne la michuano ya Europa League baada ya kuitandika Dnipro ya Ukraine katika mchezo wa fainali uliochezwa jijini Warsaw, Poland jana. Sevilla ambao pia walikuwa wakitetea taji hilo walilazimika kutoka nyuma katika mchezo huo baada ya Dnipro kutangulia kufunga bao la mapema kupitia kwa nyota wao Nikola Kalinic kabla ya kusawazisha na kuongeza lingine haraka haraka. Hata hivyo Dnipro walikuja juu na kusawazisha bao hilo na kuzifanya timu hizo kwenda mapumziko zikiwa zimetoshana nguvu kwa kufungana mabao 2-2.Alikuwa ni Carlos Bacca aliyewainua mashabiki wa Sevilla kwa kufunga bao la tatu na la ushindi katika dakika ya 73 na kuifanya timu yake kutetea taji lao hilo.Sevilla mbali na kufuzu moja kwa moja michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao pia inakuwa timu ya kwanza kunyakuwa taji hilo kwa mara nne.

No comments:

Post a Comment