Saturday, May 2, 2015

BAADA YA KUPIMA UZITO JANA USIKU SASA MAYWEATHER NA PACQUAIO WAKO TAYARI KUZICHAPA.

MABONDIA mahiri Floyd Mayweather na Manny Pacquiao wamepima uzito jana mbele ya mashabiki 11,500 waliohudhuria shughuli hiyo kuelekea katika pambano la kihistoria linalotarajiwa kufanyika jijini Las Vegas leo usiku au alfajiri ya kuamkia kesho kwa saa za hapa nyumbani. Viingilio kwa mashabiki waliofurika kushuhudia mabondia hao wakipima uzito vilikuwa dola ingawa tiketi hizo zilikuja kulanguliwa mpaka dola 800. Pambano linalotajwa kuingiza fedha nyingi katika historia linakadiriwa kutengeneza zaidi ya dola milioni 400. Mayweather wa Marekani na Pacquiao wa Philippines watakuwa wakishindania mikanda ya dunia ya WBC, WBA na WBO uzito wa welter. Akihojiwa Mayweather amecheza mapambano 47 bila kupigwa, amesema anaamini uwezo wake na mbinu zake hivyo lazima ataibuka kidedea katika pambano hilo. Kwa upande wake Pacquiao ambaye ameshinda mapambano 57 na kupigwa matano katika mapambano 64 aliyocheza, amesema ni jukumu lake kubwa kuwapa furaha mashabiki haijalishi kama mashabiki wake au wa mpinzani wake.

No comments:

Post a Comment