Saturday, May 2, 2015

VIWANJA VYA KOMBE LA DUNIA VYAKAMILIKA MIEZI BAADA YA MICHUANO HIYO.

HATIMAYE baadhi ya viwanja vya Kombe la Dunia nchini Brazil vimekamilika miezi 10 baada ya michuano hiyo kumalizika. Viwanja hivyo vilivyokamilika kufikia jinsi vilivyotakiwa ni Uwanja wa Itaquerao uliopo jijini Sao Paulo na Arena da Baixada uliopo Curitiba. Pamoja na kutokamilika kwake viwanja hivyo vyote vilitumika wakati wa Kombe la Dunia ambalo lilibebwa na Ujerumani. Brazil ilitumia zaidi ya dola bilioni 3 kwa ajili ya ujenzi wa viwanja vya michuano hiyo huku waandamanaji wakipinga kiasi kikubwa wa cha fedha zilizotumika katika ujenzi huo.

No comments:

Post a Comment