Thursday, May 21, 2015

KOCHA WA LAZIO ADAI BAHATI NDIO ILIYOWASAIDIA JUVENTUS KUNYAKUWA KOMBE LA ITALIA.

MENEJA wa klabu ya Lazio, Stefano Pioli amedai kuwa kikosi chake hakikupaswa kupoteza mchezo wao wa fainali wa Kombe la Italia na kuongeza kuwa wapinzani wao Juventus walikuwa na bahati. Juventus ilifanikiwa kunyakuwa taji hilo baada ya kushinda mabao 2-1 katika muda wa nyongeza baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika muda wa kawaida katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Olimpiki. Juventus sasa wamejiweka katika nafasi nzuri ya kunyakuwa mataji matatu kea mkupuo baada ya kuwa tayari wameshachukua lile la Serie A huku wakitarajiwa kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Barcelona Juni 6 mwaka huu. Akihojiwa Pioli amesema ulikuwa ni mchezo uliokuwa na uwiano sawa kutokana na kila timu kuwa na nafasi ya kupata ushindi lakini ilihitajika bahati kidogo jambo ambalo hawakuwa nalo katika mchezo huo. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa walistahili matokeo tofauti na hayo lakini kutoka na timu waliyocheza nayo hana jinsi zaidi ya kuwapongeza wachezaji wake kea mchezo mzuri.

No comments:

Post a Comment