Thursday, May 21, 2015

MALDINI NAYE AZINDUA TIMU YAKE MIAMI.

NGULI wa soka Italia, Paolo Maldini anatarajiwa kuhasimiana na David Beckahm baada ya kuzindua klabu yake ya soka jijini Miami, Marekani. Klabu ya Soka ya Miami inatarajiwa kucheza katika Ligi Daraja la Pili ikiwa chini ya Ligi Kuu nchini humo maarufu kama MLS. Maldini mwenye umri wa miaka 46 atakuwa mmliki mwenza katika klabu hiyo ambayo inatarajiwa kuleta upinzani kea Beckham ambaye naye anataka kuingiza timu kutoka Miami kwenye Ligi Kuu siku zijazo. Mpango huo wa Beckham ulikwama kidogo wakati mkakati wa kijenga uwanja mpya wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 25,000 ulipokataliwa mwaka jana. Beckham na Maldini wamewahi kucheza pamoja kwa kipindi kifupi mwaka 2009 katika klabu ya AC Milan.

No comments:

Post a Comment