Thursday, May 21, 2015

HABARI MBAYA KWA UNITED BAADA YA HUMMELS KUSISITIZA KUMALIZA MKATABA WAKE DORTMUND.

BEKI mahiri wa kimataifa wa Ujerumani Mats Hummels amezima tetesi za kuhamia Manchester United kea kuthibitisha kuwa anatarajia kuendelea kuitumikia Borussia Dortmund msimu ujao. Hummels mwenye umri wa miaka 26 amekaririwa na gazeti Kicker la Ujerumani akidai kuwa anataka kumaliza mkataba wake na Dortmund utakaokwisha mwaka 2017. Mkurugenzi wa michezo wa Dortmund, Michael Zorc amesema mara nyingi amekuwa akieleza kuwa Hummels yuko katika mipango yao na anashukuru mwenyewe kulifafanua hilo. Kwa kipindi kirefu United walikuwa wakihusishwa na tetesi za kumtaka beki huyo huku meneja Louis van Gaal akiripotiwa kuwa tayari kutenga kitita cha euro milioni 40 ili kupata saini yake. Lakini sasa nyota huyo ataingia katika mipango ya kocha mpya wa Dortmund Thomas Tuchel ambaye atachukua nafasi ya ya kocha wa sasa Jurgen Klopp.

No comments:

Post a Comment