Thursday, May 21, 2015

XAVI ATANGAZA RASMI KUONDOKA BARCELONA MWISHONI MWA MSIMU NA KWENDA QATAR.

KIUNGO mkongwe wa Barcelona, Xavi ametangaza nia yake ya kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu na kujiunga na klabu ya Al Sadd ya Qatar. Xavi ameitumikia Barcelona kwa kipindi cha miaka 24 toka alipojiunga nao akiwa na umri wa miaka 11 na kuwa mchezaji wa kwanza katika klabu hiyo kucheza mechi zaidi ya 750 katika kikosi cha kwanza. Ingawa amecheza zaidi ya mara 41 katika msimu huu, Xavi amekuwa akitumiwa zaidi akitokea benchi toka meneja Luis Enrique alipochukua mikoba ya kuinoa timu hiyo kiangazi mwaka jana. Akizungumza mbele ya wanahabari leo, Xavi amesema uamuzi wake huo aliochukua in mgumu sana lakini anadhani wakati wake wa kuondoka umefika. Kiungo huyo aliendelea kudai kuwa klabu hiyo ilimpa ofa nzuri ya kuongeza mkataba lakini tayari alishachukua uamuzi wa kuondoka. Xavi aliendelea kudai kuwa atakwenda kucheza katika timu ya Al Sadd ambako amesaini mkataba wa miaka miwili lakini anaweza kuongeza kama akiona muda unamruhusu kuendelea.

No comments:

Post a Comment