Thursday, May 21, 2015

WAKALA WA STERLING ADAI HATA LIVERPOOL WANGEMPA OFA YA PAUNDI 900,000 KWA WIKI ASINGESAINI MKATABA MPYA.

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Uingereza, Raheem Sterling amesema mteja hatasaini mkataba mpya na Liverpool hata kama akipewa ofa ya kulipwa paundi 900,000 kwa wiki. Wakala huyo Aidy Ward pia alimponda beki wa zamani wa klabu hiyo Jamie Carragher kwa kukosoa mpango wa Sterling kuondoka. Ward amesema hajali watu wanasemaje kwasasa kwani kitu muhimu in kuhakikisha mteja wake anapata timu ambayo atafurahia kuitumikia. Sterling bado ana mkataba na Liverpool unaomalizika mwaka 2017 na amekataa mkataba mpya ambao ungemuwezesha kulipwa kitita cha paundi 100,000 kea wiki.

No comments:

Post a Comment