Friday, May 22, 2015

MOURINHO MENEJA BORA WA MWAKA EPL.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho ameshinda tuzo ya meneja bora wa mwaka kea kuingoza timu hiyo kunyakuwa taji lake la tano la Ligi Kuu, wakati Eden Hazard akinyakuwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka. Chelsea imefanikiwa kunyakuwa taji hilo huku wakiwa bado wana michezo mitatu mkononi na wanaweza kumaliza kwa tofauti ya alama 11 na mahasimu wao kama wakishinda mchezo wa mwisho wa ligi Jumapili hii. Huu in msimu wa pili kwa Mourinho toka arejee Stamford Bridge na amepiga hatua moja mbele bada ya kuiwezesha timu hiyo kushika nafasi ya pili msimu uliopita. Pia in mara ya tatu Mourinho kunyakuwa tuzo hiyo baada ya kuwahi kunyakuwa tena msimu wa mwaka 2004-2005 na 2005-2006.

No comments:

Post a Comment