Friday, May 22, 2015

WALCOTT, RAMSEY HAWAENDI POPOTE - WENGER.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger anategemea Theo Walcott na Aaron Ramsey kubakia katika klabu hiyo katika majira ya kiangazi. Walcott amepoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza toka aliporejea kutoka katika majeruhi ya goti, wakati Ramsey amekuwa akihusishwa na tetesi za kuwindwa na klabu ya Barcelona. Hata hivyo Wenger amekanusha tetesi zozote zinzohusiana na wachezaji hao kuondoka akidai kuwa hana shaka kuwa watabakia tayari kea ajili ya msimu ujao. Walcott alitokea benchi na kutengeneza nafasi ya bao la kusawazisha katika sare ya bao 1-1 waliyopata kutoka Manchester United, lakini nyota huyo amekuwa akilalamika kupewa muda mchache wa kucheza. Pamoja na kutokuwa na furaha Wenger anaamini Walcott mwenye umri wa miaka 26 atarejea katika kikosi cha kwanza akiwa katika kiwango chake bora msimu ujao. Arsenal inatarajiwa kupambana na West Bromwich Albion katika mchezo wa mwisho wa ligi kabla ya kuvaana na Aston Villa katika fainali ya Kombe la FA Mei 30 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment