Thursday, May 21, 2015

PALESTINA YAIKOMALIA ISRAEL IONDOLEWE FIFA.

PALESTINA imesema itaendelea na juhudi zake za kutaka kusitishwa ushiriki wa Israel katika mashindano yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA. Palestina imeazimia hivyo licha ya rais wa shirikisho hilo Sepp Blatter kukutana na rais wa mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas na maafisa wa Ukingo wa magharibi jana. Blatter amesema Israel imependekeza kulegeza vizuizi vya kusafiri kwa wachezaji wa Palestina, wageni na maafisa wa michezo, zilizowekwa kutokana na matatizo ya kiusalama. Chama cha Soka cha Palestina kimeishutumu Israel kwa kuzuia shughuli za kimichezo na kuzuia wachezaji kusafiri kati ya Ukanda wa Gaza na Ukingo wa magharibi. Wajumbe watapiga kura kusitisha ushiriki wa Israel katika michezo Mei 29.

No comments:

Post a Comment