Thursday, May 21, 2015

MORENO AKIRI KUWA SHABIKI WA EUROPA LEAGUE.

BEKI wa Liverpool, Alberto Moreno amesisitiza kuwa shabiki mkubwa wa michuano ya Europa League wakati timu hiyo ikijiandaa kujihakikishia nafasi ya kushiriki michuano hiyo ya pili kwa vilabu Ulaya. Baada ya kushindwa kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao, Liverpool wanaweza kupata nafasi ya Europa League pamoja na kukabiliwa na upinzani kutoka kea Tottenham Hotspurs na Southampton kuelekea katika mechi zao za mwisho wa msimu. Kama Liverpool wakifanikiwa kuitandika Stoke City Jumapili hii watakuwa wamejihakikishia nafasi ya kushiriki michuano hiyo na Moreno angependa wafanikishe hilo. Moreno ambaye amewahi kunyakuwa taji la michuano hiyo akiwa na Sevilla msimu uliopita, amesema anaihusudu michuano hiyo ana matumaini wanaweza kupata nafasi hiyo Jumapili.

No comments:

Post a Comment