Friday, May 29, 2015

URUGUAY WATAKA SUAREZ AFUTIWE ADHABU.

UMOJA wa wachezaji nchini Uruguay umedai kuwa adhabu ya kufungiwa mechi tisa Luis Suarez kwa kosa la kumng’ata nyota wa kimataifa wa Italia Giorgio Chiellini katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka jana nchini Brazil inapaswa kuondolewa. Umoja unataka suala hilo kujadiliwa tena katika mkutano mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA utakaofanyika leo jijini Zurich, Uswisi ambapo pamoja na mambo mengine pia utafanyika uchaguzi mkuu wa kutafuta rais mpya. Hatua hiyo ya kuhoji adhabu ya Suarez inakuja kufuatia tuhuma nzito za rushwa zinalikabilishi shirikisho hilo baada ya maofisa kadhaa kukamatwa. Mshauri wa masuala ya kisheria wa umoja huo, Ernesto Liotti amesema tuhuma za rushwa zinazolikabili shirikisho hilo zinathibitisha ukweli kuwa baadhi ya maamuzi yaliyofanyika katika kipindi cha karibuni hayakuwa ya haki. Liotti amesema hawana ushahidi kuwa adhabu aliyopewa Suarez ilitolewa chini ya shinikizo la viongozi hao waliokamatwa na rushwa lakini hakuna chochote kinachowahakikishia tofauti. Liotti aliendelea kudai kuwa mmoja wa maofisa waliokamatwa, ambaye in rais wa Shirikisho la Soka la Venezuela Rafael Esquivel alikuwepo katika kamati ya nidhamu iliyotoa adhabu kea Suarez.

No comments:

Post a Comment