Friday, May 29, 2015

HERNANDEZ ALIMWA ADHABU KUFUATIA KUMPIGA PHIL JONES.

CHAMA cha Soka cha Uingereza-FA kimemlima adhabu ya kutocheza mechi tatu mshambuliaji wa Hull City Abel Hernandez kea kosa la kumpiga beki wa Manchester United Phil Jones katika mchezo baina ya timu hizo uliochezwa Jumapili iliyopita. Hernandez alifanya tukio hilo katika dakika ya 70 lakini halikuonwa na mwamuzi katika mchezo ambao Hull walipata sare ya bila kufungana ambayo iliwashusha daraja. Katika taarifa yake, FA ilithibitisha taarifa hizo na kudai kuwa Hernandez anatarajiwa kuanza kutumikia adhabu yake kuanzia msimu ujao. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya nyota huyo kukubalia kutenda kosa hilo ambalo pamoja na kuwa halikuonwa na mwamuzi lakini picha za video zilinasa. Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay alijiunga na Hull akitokea Palermo ya Italia mwaka jana kea kitita cha paundi milioni tisa lakini ameshindwa kung’aa baada ya kufunga mabao manne katika mechi 25 alizocheza za mashindano yote.

No comments:

Post a Comment