Friday, May 29, 2015

PALESTINA WAZIDI KUIKOMALIA ISRAEL.

WAANDAMANAJI wa Kipalestina walimkatisha Sepp Blatter na kutaka kadi nyekundu kwa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA wakati wa mkutano mkuu wa leo. Blatter ambaye anatarajiwa kuchaguliwa tena kuongoza FIFA kwa kipindi cha tano, alikuwa akizungumza wakati waandamanaji hao walipovamia ukumbi mkubwa wa mikutano wa Hallenstadion jijini Zurich. Wakati watu wakiwa hawajaleta vurugu zozote, Blatter aliwataka watu wa usalama kushughulikia tatizo hilo kabla hajaendelea na mkutano kea kuwakumbuka watu waliokufa katika soka kwa mwaka mzima. Baada ya hapo Blatter aliomba ukimya wa dakika moja katika kumbukumbu ya miaka 30 ya tukio lililotokea Uwanja wa Heysel ambapo watu 39 walifariki dunia. Maofisa wa Palestina hivi karibuni wameitaka FIFA kuisimamisha Israel kwa kile walichodai mamlaka za nchi hiyo kuwafanyia vitendo vya udhalilishaji katika eneo la ukanda ukanda wa Gaza wa mechi za soka.

No comments:

Post a Comment