Friday, May 29, 2015

CITY YAHIRISHA MCHEZO WAKE DHIDI YA HOUSTON DYNAMO.

KLABU ya Manchester City imeahirisha mchezo wake wa kirafiki dhidi ya timu ya Houston Dynamo ya Marekani uliokuwa uchezwe jana baada ya mafuriko yalioacha uwanjani kushindwa kuchezeka. City walisafiri kwenda Houston baada ya kushinda bao 1-0 katika mchezo mwingine wa kirafiki dhidi ya Toronto FC Jumatano, wakati mvua kubwa iliponyesha katika miji ya Texas na Oklahama. Pamoja na jitihada za wahudumu wa uwanja wa Dynamo, mkaguzi wa uwanja alidai kuwa uwanjani huyo hautakuwa salama kuchezewa. City sasa watasafiri kwenda jijini New York kutizama mchezo wa klabu yao nyingine ya New York City FC itakayovaana na Houston katika mchezo wa Ligi Kuu ya Marekani utakaofanyika katika Uwanja wa Yankee, Jumamosi hii.

No comments:

Post a Comment