Friday, May 29, 2015

PEPE ADAI BENITEZ BONGE LA KOCHA.

BEKI mahiri wa Real Madrid, Pepe amemtaja Rafa Benitez kama kocha mkubwa baada ya kukaribia kutua Santiago Bernabeu. Benitez alitangaza jana kuwa ataachia nafasi yake ya ukocha katika klabu ya Napoli, huku Madrid wakitarajiwa kumthibitisha kama mbadala wa Carlo Ancelotti wiki ijayo. Pepe anaamini kocha huyo wa Hispania ndio atakuwa chaguo la juu kwa Madrid ingawa mpaka sasa hakuna chochote kilichpafikiwa kati ya pande hizo mbili. Akihojiwa Pepe amesema benitez ni kocha mkubwa ambaye amefanya kazi nzuri popote alipokwenda haswa kaika klabu ya Liverpool. Hata hivyo Pepe alienmdelea kudai kuwa kwasasa bado ni mazungumzo katika vyombo vya habari, wacha waone kitakachotokea siku zijazo.

No comments:

Post a Comment