Friday, May 29, 2015

WILSHERE APANIA TAJI LA FA.

KIUNGO wa Arsenal, Jack Wilshere anaamini msimu wao utaamuliwa vyema kama wakifanikiwa kutetea taji lao la Kombe la FA. Arsenal imemaliza katika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu na kiungo huyo amesema utakuwa msimu mzuri kama wakifanikiwa kuichapa Aston Villa kesho katika mchezo wa fainali utakaofanyika katika Uwanja wa Wembley. Wilshere mwenye umri wa miaka 23, amesema lengo lilikuwa kumaliza katika nafasi ya pili lakini hilo halikufanikiwa hivyo itakuwa vyema zaidi kama wakimaliza kwa kubeba walau Kombe la FA. Kiungo huyo alikosa sehemu kubwa ya msimu, kufuatia kuumia kifundo cha mguu katika mchezo dhidi ya Manchester United Novemba mwaka jana na kukiri kuwa alikuwa mpweke katika kipindi chote alipokuwa peke yake gym wakati wenzake wanafanya mazoezi.

No comments:

Post a Comment