Tuesday, June 2, 2015

BADO SIJAJUA MUSTAKABALI WANGU MSIMU UJAO – BENTEKE.

MSHAMBULIAJI wa Aston Villa Christian Benteke amesema atamuachia wakala wake mustakabali wake kufuatia tetesi za kutakiwa na klabu za Liverpool na Chelsea.Benteke mwenye umri wa miaka 24, alikuwa amewavutia wengi msimu huu kutoka na kiwango chake huku Chelsea wakiwa tayari kuingia katika mbio hizo pamoja na Liverpool kumsajili mshambuliaji huyo ambaye amemaliza msimu akiwa amefunga mabao tisa katika mechi 10 za mwisho alizocheza.Wakati Benteke akikiri kuwa hadhani kama atakuwepo Villa msimu ujao lakini nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji amesisitiza kuwa atajiunga katika klabu ambayo itamuhakikishia nafasi ya kucheza mara kwa mara.Akihojiwa na luninga ya Sky, Benteke amesema kwasasa anamuachia shughuli hiyo wakala wake kwani yeye ndio anafahamu kitu gani anataka.

No comments:

Post a Comment