Tuesday, June 2, 2015

LIVERPOOL YAMTOLEA MACHO MILNER.


KLABU ya Liverpool inajipanga kufanya mazungumzo na kiungo wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Manchester City James Milner wiki hii.Liverpool imeamua kuupa kipaumbele uhamisho wa kiungo huyo aiyemaliza mkataba wake City na wana uhakika wanaweza kuafikiana.Kama mambo yote yakienda sawa, Milner mwenye umri wa miaka 29 ambaye alihamia City akitokea Aston Villa mwaka 2010, atajiunga rasmi na Liverpool Julai mosi mwaka huu.Milner alianza soka lake kaika klabu ya nyumbani kwao ya Leeds United kabla ya pia kuitumikia Newcastle United kwa miaka minne.Akiwa City Milner amefanikiwa kunyakuwa taji la Ligi Kuu mara mbili na moja la FA katika kipindi cha miaka mitano aliyokuapo hapo.

No comments:

Post a Comment