Monday, June 29, 2015

COSTA ATHIBITISHA KUTAKIWA NA BAYERN.

KIUNGO wa kimataifa wa Brazil, Douglas Costa leo amethibitisha nia ya mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich kutaka kumsajili lakini amedai hakuna dili lolote lililoafikiwa mpaka sasa. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 ambaye anakipiga katika klabu ya Shakhtar Donetsk ya Ukraine amesema mazungumzo yanaendelea kufanyika kati ya klabu hizo mbili. Bayern wanataka kumsajili kiungo huyo ambaye pia anaweza kucheza kama winga kutokana na wasiwasi wa majeruhi ya muda mrefu wa mawinga wake Franck Ribery na Arjen Robben. Akihojiwa Costa amesema anafahamu kuwa mazungumzo kati ya klabu yake na Bayern yamefanyika lakini hajui kinachoendelea zaidi kufahamu Bayern wanataka kumsajili.

No comments:

Post a Comment