Wednesday, June 24, 2015

LIVERPOOL YAKAMILISHA USAJILI WA FIRMINO.

KLABU ya Liverpool, imefanikiwa kuinasa saini ya mshambuliaji Roberto Firmino kutoka timu ya Hoffenheim kwa kitita cha paundi milioni 29. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya baada ya kurejea kutoka Chile ambako anaitumikia Brazil katika michuano ya Copa America. Firmino ambaye amefunga mabao 49 katika mechi 153 alizoichezea Hoffenheim anakuwa mchezaji wa pili ghali kuwahi kusajiliwa na Liverpool. Liverpool iliwahi kuweka rekodi yake ya usajili kwa Andy Carroll ambaye alijiunga nao kwa kitita cha paundi milioni 35 akitokea klabu ya Newcastle United mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment