Wednesday, June 24, 2015

PELLEGRINI AMPONDA MOURINHO.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amemponda hasimu wake Jose Mourinho akidai meneja huyo wa Chelsea anapenda kusifiwa kea kila kitu. Mourinho ameingoza Chelsea kunyakuwa taji la Ligi Kuu msimu uliopita, wakimaliza kea alama nane mbele ya City walioshika nafasi ya pili. Lakini Pellegrini anaamini tabia ya jinsi wao wawili wanavyosheherekea ubingwa unaonyesha kea kiasi walivyo tofauti huku kocha huyo raia wa Chile akimtuhumu Mourinho kutotambua mchango wa wachezaji wake. Akihojiwa kuhusiana na hilo Pellegrini amesema wakati Mourinho akishinda anataka sifa zote apewe yeye hali ambayo in tofauti kwake kwani aliposhinda taji hilo hakusema lolote. Hata hivyo kocvha huyo aliongeza kuwa hana tatizo lolote na Mourinho na pia sio adui yake lakini anaamini wanatofautiana kea kiasi kikubwa.

No comments:

Post a Comment