Wednesday, June 24, 2015

ROMA YAMNASA BERTOLACCI.

KLABU ya AS Roma imetangaza rasmi katika mtandao wake kuwa imemnyakuwa moja kwa moja Andrea Bertolacci kwa kitita cha euro milioni 8.5. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 alikuwa akimilikiwa nusu na Roma pamoja na timu ya Genoa ambayo ameitumikia katika misimu mitatu iliyopita. Hata hivyo, nyota huyo sasa amepata nafasi ya kurejea tena Roma kufuatia kuonyesha kiwango bora akiwa na Genoa. Katika taarifa yake Roma ilithibitisha taarifa hizo za kumsajili moja kwa moja Bertolacci ambaye ameanzia soka lake katika shule ya michezo ya klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment