Wednesday, June 24, 2015

RENARD AMTAKA JORDAN AYEW LILLE.

MENEJA wa klabu ya Lille, Herve Renard amedai kuwa mshambuliaji wa kimataifa wa Ghana Jordan Ayew anataka kuikacha klabu ya Loriente na kujiunga na timu yake. Renard amewahi kufanya kazi na Ayew wakati akiinoa klabu ya Sochaux ambako kinda huyo alikuwa akicheza kwa mkopo akitokea Olimpique Marseille. Wawili hao walitengeneza mahusiano ya karibu kati yao na sasa baada ya Renard kuchukua kibarua Lille anataka kumsajili nyota huyo. Akihojiwa Renard amesema ana uhakika Ayew anataka kujiunga na kikosi chake lakini ana viongozi wake ambao ndio wataamua mustakabali wake.

No comments:

Post a Comment