Monday, June 29, 2015

RONALDO APANIA KUJITANGAZA ZAIDI BARANI ASIA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amebanisha kuuza sehemu ya haki ya kutumia picha zake kwa mmiliki wa klabu ya Valencia Peter Lim ili kukuza jina lake barani Asia. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 30, hivi karibuni alitajwa kuwa wa tatyu katika orodha ya wanamichezo matajiri duniani na sasa anajipanga kuongeza utajiri wake zaidi. Ronaldo mwenyewe ambaye ana urafiki wa karibu na bilionea huyo wa Valencia, alithibitisha taarifa hizo kupiti mtandao wake wa kijamii wa facebook akidai kuwa hatua hiyo ni muhimu kwake kwa kulikuza jina lake kimataifa. Kampuni ya Mint Media yenye makao yake huko Hong Kong na kumilikiwa na Lim, ilidai katika taarifa yake kuwa mkataba wa miaka sita waliosaini na Ronaldo utasaidia kukuza jina la nyota huyo barani humo.

No comments:

Post a Comment