Monday, June 29, 2015

CITY YAMUWINDA FABINHO.

KLABU ya Manchester City inajipanga kumuwania beki wa kulia wa klabu ya AS Monaco ya Ufaransa Fabinho. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 alikuwepo katika kikosi cha Brazil chini ya kocha Dunga kwenye michuano ya Copa America nchini Chile ingawa hakucheza katika mechi yeyote. Pamoja na kuwa hakuna mazungumzo yeyote yaliyoanza mpaka sasa, inaaminika City wamekuwa wakifuatilia nyendo za beki huyo katika wiki za karibuni. Beki huyo ambaye pia amekuwa akidaiwa kuwindwa na klabu za Chelsea na Manchester City, Monaco wamepanga kumuuza kwa kitita cha euro milioni 25.4 kwa timu itakayomuhitaji.

No comments:

Post a Comment