Friday, July 31, 2015

CHELSEA VS ARSENAL NGAO YA JAMII JUMAPILI.

PAZIA la Ligi Kuu nchini Uingereza, linatarajiwa kufunguliwa mwishoni mwa wiki kwa mchezo wa Ngao ya Jamii utakaozikutanisha timu za Chelsea na Arsenal zote kutoka jijini London. Mchezo huo ambao utachezwa Jumapili hii katika Uwanja wa Wembley huzikutanisha timu ambazo ni mabingwa katika Ligi Kuu pamoja na Kombe la FA. Chelsea wao ndio waliibuka mabingwa wa ligi msimu uliopita huku Arsenal wao wakifanikiwa kutetea taji lao la FA kwa mara ya pili na kuweka historia kuwa timu ya kwanza kunyakuwa taji hilo mara nyingi zaidi. Ligi rasmi inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 8 mwaka huu kwa michezo nane ambapo Manchester United watakuwa wenyeji wa Tottenham Hotspurs katika Uwanja wa Old Trafford huku Bournemouth ambao wamepanda daraja msimu huu wao wakiikaribisha Ason Villa. Nyingine ni Norwich City watakaokuwa wenyeji wa Crystal Palace, Leicester City dhidi ya Sunderland, Everton dhidi ya Watford na mabingwa Chelsea dhidi ya Swansea City.

No comments:

Post a Comment