Tuesday, July 21, 2015

PELE ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI.

NGULI wa soka wa Brazil, Pele ameruhusiwa kutoka hospitali baada ya kufanyiwa upasuaji wa mgongo uliofanikiwa. Nguli huyo mwenye umri wa miaka 74 alikuwa akisumbuliwa na maumivu makali ya mgongo na lifanyiwa upasuaji huo katika hospitalia ya Albert Einstein iliyopo jijini Sao Paulo. Pele ambaye amewahi kushinda taji la Kombe la Dunia mara tatu akiwa na Brazil, amewahi kutibiwa maambukizi katika njia ya mkojo miezi nane iiyopita baada ya kuondolewa mawe katika figo. Pele amefanikiwa kucheza mechi 14 katika Kombe la Dunia akifunga mabao 12 na alitunukia tuzo mpira wa dhahabu kama mchezaji bora wa mashindano mwaka 1970.

No comments:

Post a Comment