Tuesday, July 21, 2015

VAN GAAL KUMTUMIA ROONEY KAMA MSHAMBULIAJI MSIMU UJAO.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal amesema amepanga kumtumia Wayne Rooney kama mshambuliaji wa kati msimu ujao. Rooney mwenye umri wa miaka 29, amekuwa akitumika katika nafasi ya kiungo katika kipindi kirefumsimu uliopita. Akizungumza na wanahabari, Van Gaal amesema amekuwa akisikiliza maoni yao kwani wamekuwa wanaufahamu zaidi yake hivyo atamtumia Rooney katika nafasi ya ushambuliaji zaidi msimu ujao. Mara ya mwisho Rooney kucheza kama mshambuliaji msimu wa 2011-2012, alifanikiwa kufunga mabao 34 na ana matumaini msimu ujao ataweza tena kufanya hivyo. Akihojiwa Rooney amesema ana matumaini ya kufunga mabao 20 au zaidi na kama akishindwa kufanya hivyo ni jambo ambalo litamhuzunisha.

No comments:

Post a Comment