Saturday, July 18, 2015

SCHNEIDERLING APIGA BAO PEKEE KATIKA USHINDI MWEMBAMBA WA UNITED HUKO MAREKANI.

KIUNGO mpya wa Manchester United, Morgan Schneiderling amefunga bao lake la kwanza akiwa mchezaji wa timu hiyo katika ushindi wa bao 1-0 walioupata dhidi ya Club America katika mchezo wa kirafiki uliofanyika huko Marekani jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa, ambaye alikamilisha usajili wake uliogharimu kitita cha dola milioni 39 kutoka Southampton mapema mwezi huu alifunga bao hilo kwa kichwa katika dakika ya tano ya mchezo. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, meneja wa United Louis van Gaal amesema wachezaji wote walicheza kama alivyowaelekeza katika kipindi chote cha mchezo hivyo anafurahi kwamba wameibuka washindi. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa jambo lingine lililomfurahisha ni safu yake ya ulinzi kutoruhusu bao kwani hiyo ilikuwa sehemu ya malengo yao.


No comments:

Post a Comment