Tuesday, August 25, 2015

BALOTELLI ADAI KUFURAHIA KUREJEA SERIE A.

MSHAMBULIAJI nyota wa Liverpool, Mario Balotelli amesema anajisikia furaha kurejea Serie A baada ya kukamilisha vipimo vya afya tayari kwa uhamisho wake wa mkopo kwenda AC Milan. Nyota huyo wa kimataifa wa Italia alitua Milan mapema leo ili kukamilisha hatua za mwisho za mkopo wake huo. Akizungumza na wanabahari mara baada ya kufanyiwa vipimo vya afya Balotelli amesema amefurahi kurejea na yuko fiti anachosubiri sasa ni kuanza mazoezi na wenzake. Nyota huyo mwenye maneno na vibwanga vingi ndani na nje ya uwanja safari hii amesema hataki kuongea sana bali kufanya kazi iliyomleta hapo. Balotelli ambaye amefunga bao moja pekee katika mechi 16 za Ligi Kuu alizocheza msimu uliopita, alikuwa ameondolewa katika mipango ya meneja Brendan Rodgers.

No comments:

Post a Comment